Samuel Umtiti kuelekea Manchester United


Mchezaji wa  wa klabu ya Barcelona  na  timu ya taifa ya Ufaransa, Samuel Umtiti huwenda akaondoka Nou Camp na kuelekea Manchester United  kwa dau la pauni milioni 50.

Umtiti huwenda akatimkia kwa mashetani hao wekundu kufuatia kukwama kwa mazungumzo ya mkataba wake na mabosi zake wa Barcelona.

Mchezaji huyo raia wa Ufaransa mara kadhaa amehusishwa kuamia Old Trafford na mpango huo kuonekana kukamilika baada ya Barcelona kukataa kumlipa anachohitaji.

Kwa mujibu wa vyombo vya habari vya michezo nchini Hisania, mchezaji huyo wazamani wa Lyon anahitaji kuwa wapili katika viwango vya mshahara ndani ya kikosi cha Barca nyuma ya Andres Iniesta na Luis Suarez.

Mpya zaidi Nzee zaidi