BREAKING: Basi la Abood lateketea kwa moto


Taarifa za hivi punde zinaeleza kuwa basi la abiria, mali ya Kampuni ya Abood limeteketea kwa moto.

Ajali hiyo ya moto imetokea eneo la Chalinze mkoani Pwani wakati basi hilo likiwe kwenye safari zake, hadi sasa chanzo cha ajali hiyo bado hakijajulikana.

Hakuna abiria aliyeripotiwa kuumia ingawa wengi wameonekana wakikimbia huku na kule kuokoa uhai wao. Endelea kuwa karibu na Muungwana Blog ili kupata habari zaidi kuhusiana na tukio hilo.