https://monetag.com/?ref_id=TTIb Msemaji wa Simba SC, Haji Manara awafungia kazi Al Ahly | Muungwana BLOG

Msemaji wa Simba SC, Haji Manara awafungia kazi Al Ahly


Msemaji wa wekundu wa msimbazi, Simba SC, Haji Manara ameeleza kuwa anaamini timu hiyo leo itacheza kwa kujilinda zaidi dhidi ya Al Ahly kutoka nchini Misri.

Utakumbuka katika michezo miwili iliyopita Simba SC wameruhusu kufungwa magoli 10 katika hatua hiyo ya makundi Ligi ya Mabingwa Afrika.

"Naamini safu yeti ya ulinzi na Aishi (mlinda mlango) leo watafanya hivyo,ni kuongeza kumakinika kwa asilimia 100," ameeleza Haji Manara.

Simba SC leo itashuka kwenye dimba la uwanja wa taifa Dar es Salaam kuivaa timu ya Al Ahly  kutoka nchini Misri. Mchezo wa awali timu hizo kukutana, Simba ilijikuta ikipoteza kwa kuzabwa magoli 5-0.