Basi la abiria, mali ya Kampuni ya Abood lenye namba za usajili T 877 DJP limeteketea kwa moto. Basi hilo ambalo linafanya safari zake kati ya Dar es Salaam na Morogoro
Ajali hiyo ya moto imetokea eneo la Chalinze mkoani Pwani karibu na mzani wa Vigwaza, hadi sasa chanzo cha ajali hiyo bado hakijajulikana.
Hakuna abiria yeyote aliyeripotiwa kuumia ingawa wengi wameonekana wakikimbia huku na kule kuokoa uhai wao. Endelea kuwa karibu na
Muungwana Blog ili kupata habari zaidi kuhusiana na tukio hilo.