Tarehe ya Uchaguzi Yanga SC yapanguliwa na TFF


Uchaguzi wa Yanga SC unatarajiwa kufanyika Mei 5 mwaka huu na Fomu zitaanza kutolewa Kesho Makao Makuu ya Klabu hiyo. Mwenyekiti wa Kamati ya Uchaguzi ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) Malangwe Ally Mchungahela ndiye ametangaza tarehe hiyo.

Awali uchaguzi huo ulitangazwa kufanyika Aprili 28 lakini kutokana na siku hiyo itakuwa fainali ya michuano ya Afrika kwa vijana chini ya miaka 17.

Ratiba kamili ya uchaguzi wa Yanga.

Aprili 2-7 kuchukua fomu

Aprili 9 Kikao cha mchujo kwa wagombea

Aprili 10 kubandikwa kwa majina yaliyopitishwa

Aprili 11-14 Pingamizi kwa wagombea

Aprili 16-18 Kupitia pingamizi na usaili

Aprili 18-23 Sekretariati kusikiliza maamuzi ya kamati ya maadili

Aprili 24-26 Kukata rufaa

Aprili 27-29 kusikiliza rufaa

Aprili 30- Mei 4 Kampeni

Mei 5 uchaguzi mkuu
Mpya zaidi Nzee zaidi

Popular Items