Basi la Abood lapata ajali likielekea Dar


Basi la kampuni ya Abood linalofanya safari zake Mwanza-Dar, limepata ajali mapema asubuhi katika eneo la Mkolani jijini Mwanza njiani likielekea Dar.

Inadaiwa kwamba chanzo cha ajali hiyo ni mwendesha pikipiki aliyekatiza barabara ghafla na kusababisha dereva wa basi kupoteza muelekeo. Muendesha piki piki huyo, amepoteza maisha huku majeruhi wakiwa wamepelekwa hospitali mbali mbali.