Wesley Sneijder astaafu kucheza soka


Kiungo wa zamani wa Real Madrid, Inter Milan na Uholanzi, Wesley Sneijder amestaafu baada ya soka ya miaka 17. Sneijder amechukua jukumu jipya na kilabu yake ya nyumbani ya FC Utrecht

Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 35 aliichezea Uholanzi kwa rekodi ya mara 134 na alionekana kwenye fainali za Kombe la Dunia mwaka 2010.

Katika kazi ya kutwaa mataji, alishinda taji la 'La Liga' huko Hispania akiwa na Real Madrid na kuendelea kushinda 'Serie A', Ligi ya Mabingwa Ulaya na Coppa Italia mara tatu akiwa Inter Milan mnamo 2009-10. .