https://monetag.com/?ref_id=TTIb Beki wa Manchester United aendelea na matibabu nchini China | Muungwana BLOG

Beki wa Manchester United aendelea na matibabu nchini China


Beki wa Manchester United Diogo Dalot ambaye ameumia, amekuwa akipatiwa matibabu katika klabu ya Shanghai SIPG ya nchini China chini ya daktari wa viungo Mbrazili anayejulikana kama daktari wa miujiza.

Beki huyo Mreno mwenye umri wa miaka 20 bado hajacheza mechi yoyote msimu huu na kocha wa mashetani hao wekundu Ole Gunner Solskjaer amesema mwezi uliopita kuwa mchezaji huyo yuko nje ya uwanja hadi baada ya mapumziko ya mechi za kimataifa.

Dalot alitua Shanghai Agosti 29 mwaka huu na kutumia siku kumi pamoja na mabingwa hao wa soka wa China.