Mwanamume mmoja kutoka Mali pia alihukumiwa kifo huku mwengine kutoka Guinea akihukumiwa kifungo cha maisha kwa kupanga na kuwasilisha sanduku hilo. Hii ni kulingana na mahakama moja ya Guangzhou iliyoshughulikia kesi hiyo.
Takuma Sakuragi alikanusha mashtaka hayo na anapanga kukata rufaa. Hii ni kulingana na wakili wake mwenye makao yake mjini Guangzhou, Chen Weixiong ambaye anasema hakukuwa na ushahidi wa kutosha kuthibitisha kuwa Sakuragi alikuwa amebeba sanduku hilo huku akihamu kama amebeba dawa za kulevya.
Kulingana na Chen, rafiki yake kutoka Nigeria alimuomba Sakuragi kumpelekea sanduku hilo nchini Japan lililoonekana kujaa viatu.
