Picha: Mama Samia asaini kitabu cha maombolezo kufuatia kifo cha aliyekuwa Mfalme wa Oman

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akisaini  kitabu cha kumbukumbu ya maombolezo kufuatia kifo cha aliyekuwa Mfalme wa Oman Hayat Qaboos bin Said  katika Ofisi ya Ubalozi wa Oman Mikocheni Jijini Dar es salaam leo Januari 16,2020. kulia Balozi wa Oman Nchini Mhe. A;li Bin Almahroqi.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akisalimiana na kumfariji Balozi wa Oman Nchini Tanzania Mhe. Ali Almahroqi alipofika katika Ofisi ya Ubalozi wa Oman Mikocheni Jijini Dar es salaam leo Januari 16,2020 kwa ajili ya kusaini kitabu cha kumbukumbu ya maombolezo kufuatia kifo cha aliyekuwa Mfalme wa Oman Hayat Qaboos bin Said. 


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akizungumza na Balozi wa Oman Nchini Tanzania Mhe. Ali Almahroqi kwenye Ofisi ya Ubalozi wa Oman Mikocheni Jijini Dar es salaam Januari 16,2020 alopofika katika Ofisi hiyo kwa ajili ya kusaini kitabu cha kumbukumbu ya maombolezo kufuatia kifo cha aliyekuwa Mfalme wa Oman Hayat Qaboos bin Said.