Sudan Kusini Jumamosi imefungua ukurasa mpya baada ya viognozi hasimu kuunda serikali ya mseto ambayo wafuatiliaji wengi wa hali nchini humo wanatumai itadumu.
Siku moja baada ya rais Slava Kiir kuivunja serikali iliyokuwepo, kiongozi wa upinzani Riek Machar aliapishwa kuwa makamu wa rais, muundo ambao ulishindwa kufanya kazi mara mbili na kuitumbukiza nchi hiyo kwenye mzozo wa vita uliowauwa karibu watu 400,000.
Sudan Kusini, taifa changa kabisa duniani ilitumbukia kwenye vita vya wenyewe kwa wenyewe mwaka 2013 baada ya wafuasi wa Kiir na Machar kuingia kwenye makabiliano makali miaka miwili tangu iliposhinda harakati za kudai uhuru kutoka Sudan.
Mbinyo kutoka jumuiya ya kimataifa uliwezesha kupatikana kwa makubaliano ya amani ya mwaka 2018.
Katika kisa cha nadra kiongozi wa kania katoliki duniani Papa Francis aliibusu miguu ya Kiir na Machar na watolea wito wa kumaliza uhasama wakati walipomtembelea mjini Vatican mwaka uliopita.
Sherehe za kuundwa serikali mpya mjini Juba zilianza kwa viongozi hao kukabidhiwa picha ya tukio hilo ile iwe iwakumbushe wajibu walio nao.
Siku moja baada ya rais Slava Kiir kuivunja serikali iliyokuwepo, kiongozi wa upinzani Riek Machar aliapishwa kuwa makamu wa rais, muundo ambao ulishindwa kufanya kazi mara mbili na kuitumbukiza nchi hiyo kwenye mzozo wa vita uliowauwa karibu watu 400,000.
Sudan Kusini, taifa changa kabisa duniani ilitumbukia kwenye vita vya wenyewe kwa wenyewe mwaka 2013 baada ya wafuasi wa Kiir na Machar kuingia kwenye makabiliano makali miaka miwili tangu iliposhinda harakati za kudai uhuru kutoka Sudan.
Mbinyo kutoka jumuiya ya kimataifa uliwezesha kupatikana kwa makubaliano ya amani ya mwaka 2018.
Katika kisa cha nadra kiongozi wa kania katoliki duniani Papa Francis aliibusu miguu ya Kiir na Machar na watolea wito wa kumaliza uhasama wakati walipomtembelea mjini Vatican mwaka uliopita.
Sherehe za kuundwa serikali mpya mjini Juba zilianza kwa viongozi hao kukabidhiwa picha ya tukio hilo ile iwe iwakumbushe wajibu walio nao.
