JPM ampandisha cheo Brigedia Jenerali Mbungo kuwa Mkurugenzi mkuu wa TAKUKURU


Rais  wa Jamuhuri ya muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli amempongeza kaimu kamishna mkuu wa Mamlaka ya kuzuia na kupambana na rushwa TAKUKURU Brigadia Jenerali Mbungo kwa kuokoa shilingi bilioni 8.8 na  kumpandisha cheo kuwa mkurugenzi wa taasisi hiyo.

“Nawapongeza TAKUKURU mmeweza kurudisha Billion 8.8 za Wananchi, tena nafikiri Brigedia Jenerali John Mbungo hautakiwi tu kuwa Kaimu (Mkurugenzi Mkuu TAKUKURU) kuanzia leo wewe nakupandisha nafasi utakuwa mkurugenzi unafanya kazi vizuri kama umerudisha Billion 8.8 utarudisha na Mabillion mengine”-JPM