Virusi vya Corona: Watu 562 wamefariki nchini Ufaransa

Watu 562 wamekwishafariki nchini Ufaransa  huku wengÅŸne 1525 wakiwa maututi hospitali.

Nchini Ufaransa  watu  562 wamekwishafariki na wengine  112 wamefariki  katika muda wa masaa  24.

Idadi ya watu waliofariki  nchini humo imefikia watu 562 amefahamisha waziri wa afya Jumamosi.

Watu 6172 wamelazwa hospitali huku wengine  1525 wakiwa katika hali maututi.

Muhusika katika idara ya afya nchini Ufaransa amezungumza na wanahabari na kusema kuwa corona imekuwa janga kubwa hivyo basi hakuna budi kuongeza juhudi za kukabiliana na virusi hivyo kwa hali na mali.

Hayo ameyazungumza  Jumamosi katika mkutano  kuhusu Covid-19.