Wanasiasa waliojitosa kupambana na corona kwa njia ya nyimbo

Tangu mlipuko wa coronavirus ulipoanza juhudi mbali mbali za kuzuwia kusambaa kwa virusi hivyo zimekua zikifanyika, lakini baadhi ya wanasiasa hawa wamejitosa kutumia usanii kuwaelemisha raia juu ya kuepuka virusi.

Rais wa Liberia na mchezaji kandanda maarufu wa zamani George Weah, tayari ametoa wimbo wake wake wa Corona aliourekodi katika studio yake mwenyewe binafsi iliyopo nyuma ya kanisa, katika mji mkuu Monrovia, kulingana na shirika la habari la Ufaransa RFI.

Alianza kuiandaa single yake ya coronavirus hata imewafiki imewafikia Waliberia, amenukuliwa msemaji wake Solo Kelgbeh akisema katika gazeti la the Guardian.

Katika wimbo wake Bwana Weah anaongea zaidi kuliko kuimba, ambapo mistari ya maneno yake imejaa taarifa kamili za elimu kuhusu jinsi ya kudhibiti kusambaa kwa virusi vya corona na dalili zake.

Katika wimbo wake alishauri kwamba jambo kuu muhimu unaloweza kufanya kujilinda mwenyewe ni kunawa mikono.

Halafu anaimba nusu ya kibwagizo : "Covid-19 inaweza kusababisha matatizo makubwa ya mfumo wa kupumua."

Kibwagizo cha wimbo huo kinaimbwa na waimbaji wa nyimbo za dini wanaoimba: "Lazima tuamke, njooni tuamke pamoja tupambane na corona ."

Wine, ambaye jina lake halisi ni Robert Kyagulanyi, ameshirikiana na msanii mwenzake Nubian Li kutoa wimbo huo Jumatano ulioimbwa kwa mtindo wa rhumba akielezea umuhimu wa usafi binafsi.

" Habari mbaya ni kwamba kila mmoja anaweza kuwa muathiriwa," Wine ameimba. "Lakini habari njema ni kwamba kila mtu anaweza kuwa suluhu."

Wawili hao wametumia wimbo wao kuwahamasisha watu kunawa mikono mara kwa mara, watu kuacha kukaribiana na kuchunguza dalili za virusi kama vile homa na kikohozi.
Mpya zaidi Nzee zaidi