Rostam Aziz atoa msaada wa mashine maalum ya kujikinga na corona Bungeni

Spika wa Bunge la jamhuri ya muungano wa Tanzania Job Ndugai ameishukuru kampuni ya Taifa Ges inayomilikiwa na Rostam Azizi kwa kuwapatia msaada wa mashine mbili za kusanitaize wabunge pamoja na wageni watakaoingia bungeni.

"Kampuni ya Taifa Gas ambayo kiongozi wake ni Mbunge mwenzetu wa zamani, Rostam Azizi wamekuja hapa Bungeni kutupatia mashine mbili ambazo zitasaidia kusanitize waheshimiwa Wabunge, wafanyakazi wa Bunge na wageni wote ambao wanatembelea hapa Bungeni"-Spika wa Bunge Job Ndugai
Mpya zaidi Nzee zaidi