https://monetag.com/?ref_id=TTIb Uturuki yatoa msaada wa vifaa vya matibabu nchini Iraq | Muungwana BLOG

Uturuki yatoa msaada wa vifaa vya matibabu nchini Iraq

Uturuki yatoa msaada wa vifaa vya matibabu nchini Iraq  kama ishara ya  ushirikiano
Uturuki imetuma vifaa vya matibabu na madawa nchini Irak kuonesha ushirikiano katika  kukabiliana na maambukizi ya virusi vya corona.

Balozi wa Uturuki mjini Baghdad nchiniIrak Fatih Yılmaz  amesema kuwa msaada  huo umetolewa nchini humo kwa lengo la kupunguza  athari  za maambukizi   na kuzuia maambukizi kuendelea katika jamii.

Msaada huo wa madawa na vifaa vya  matibabu ni kwa ajili ya hospitali za zahanati ambazo zimekumbwa na uhaba wa madawa.

Balozi huyo wa Uturuki nchini humo Iraq amenndelea akisema kwamba katika kipindi hiki kigumu cha kupambana na maambukizi ya virusi vya corona , Uturuki imejitolewa   kadri na uwezo waek kuwa karibu na mataifa ambayo yalihitaji msaada katika kupambana na covid-19.

Wakti ambapo visa vipya vikiendelea kuripotiwa nchini humo  , idara ya afya imekumbwa na changamoto kubwa kutokana na uhaba wa vifaa vya matibabu.

Kutokana na uhaba huo, waziri  mazingira na jamii ameomba msaada kutoka Uturuki ilikuweza kumudu  ombi kubwa la madawa katika hospitali tofauti.

Rais ErdoÄŸan amesema kwamba ni jukumu kwa Uturuki kuonesha  ushirikiano na majirani zake katika kukabiliana na janga la corona.

Ni watu  839 nchini Irak ambao wamekwishafariki kutokana na maambukizi ya virusi vya corona  huku  watu walioambukiwa idadi yake ikitajwa kuwa watu  47 151.