Aliyekua Mkuu wa Wilaya ya Kongwa amechukua fomu kugombea Ubunge Jimbo la Chilonwa

Aliyekua Mkuu wa Wilaya ya Kongwa, Deo Ndejembi amechukua fomu ya kuomba nafasi ya kuteuliwa kugombea Ubunge Jimbo la Chilonwa wilaya ya Chamwino, Dodoma kupitia Chama cha Mapinduzi.

Akizungumza mara baada ya kuchukua fomu Ndejembi amemshukuru Rais Magufuli kwa kumuamini katika nafasi ya u-DC kwa miaka minne.