Majaliwa achukua fomu ya kuwania tena Ubunge wa Ruangwa

 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akikabidhiwa  fomu za kuwania tena ubunge wa jimbo la Ruangwa na Katibu wa CCM wa wilaya  ya Ruangwa, Barnabas Essau kwenye Ofisi ya CCM ya wilaya hiyo, Julai 15, 2020. Kushoto ni mkewe Mary Majaliwa.

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akitia saini kitabu baada ya kurejesha fomu za kuwania tena Ubunge wa Jimbo la Ruangwa, Julai 15, 2020. Kulia ni Katibu wa CCM wa wilaya ya Ruangwa, Barnabas Essau.

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akionyesha fomu za kuwania tena Ubunge wa Jimbo la Ruangwa baada ya kuzichukua, kuzijaza na kuzirejesha, Julai 15, 2020. Kushoto ni Mkewe Mary Majaliwa.