https://monetag.com/?ref_id=TTIb “Rais Magufuli akikupenda atakutoa kwa heshima” Kigwangalla | Muungwana BLOG

“Rais Magufuli akikupenda atakutoa kwa heshima” Kigwangalla


Waziri wa Maliasili na Utalii Dr. Hamis Kigwangalla leo July 1, 2020 amefanya mahojiano na kituo cha TV cha Clouds TV ambapo hapa nakusogezea nukuu mbili alizoongea leo.

“Rais Dkt John Magufuli akikupenda sana atakutoa kwa heshima atakusemea mambo mengine hayo mengine hayasemi na ukiona upo kwenye wizara muda mrefu ujue yeye na vyombo vyake wanakufuatilia hadi wanajiridhisha huyu mtu hapigi pesa” -Hamisi Kigwangalla

“Kuna vingi unatarajia vifanyike kwenye Utalii ila kuna taratibu za Serikali zitakuzuia tu,utatamani utoe tiketi 5 lakini utaulizwa hizi tiketi zilikuwa kwenye bajeti gani,kifungu gani tayari utaambia matumizi mabaya ya ofisi tayari ni tatizo pale”– Hamis Kigwangalla