Jumuiya ya Machifu mkoani Mbeya imesema bado wanawake na watoto kwenye baadhi ya familia wanakosa haki zao za msingi ikiwamo umiliki wa mali, haki ya kupata elimu na fursa za mbalimbali za uongozi kwa sababu ya kuendekeza mfumo dume.
Hayo yamebainishwa na Chifu wa Kabila la Wasafwa mkoani Mbeya Roketi Mwashinga, na Chifu Msaidizi wa kabila hilo George Lyoto, ambao wote wamesema kuwa unampoamua kumnyanyasa mwanamke, unamnyima nguvu na kumdidimiza hali inayopelekea yeye kujiona ni dhaifu na hama maamuzi.
Kwa upande wake Mchungaji Marry Kategile ambaye ni Mkurugenzi wa Elimu Anuai kutoka Chuo Kikuu cha Teofilo Kisanji (TEKU), ambapo wamesema kuwa ukatili wa kijinsia bado ni mkubwa na hata usawa wa kijinsia katika masuala ya kiongozi wanawake ni wachache.
