Membe: Nimepima afya yangu Dubai, nipo imara kuendelea na kampeni

 


Mgombea urais wa Tanzania kwa tiketi ya ACT-Wazalendo, Bernard Membe amerejea nchini Septemba 15, 2020 akitokea Dubai baada ya kumaliza shughuli zake huko na kwamba yupo imara kuendelea na kampeni za uchaguzi mkuu.

Membe amesema alikuwa Dubai kwa sababu za kibiashara kwani yeye ni mjumbe wa bodi ya kampuni kubwa mjini humo na hakuweza kuhudhuria vikao viwili mfululizo kutokana na mlipuko wa virusi vya corona.

Aidha, ameongeza kuwa, akiwa Dubai alitumia fursa hiyo kufanya uchunguzi wa kiafya na yeye ni mzima wa afya na yupo tayari kuendelea na kampeni.

Post a Comment

0 Comments