Waziri Mkuu wa Msumbiji Carlos Agostinho do Rosario amesema watu zaidi ya 500,000 wamelazimika kuhama makazi yao kwasababu ya wanamgambo wa Kiislamu katika eneo lenye utajiri wa gesi kaskazini mwa mkoa wa Cabo Delgado.
Jumatano , waziri huyo ameliambia bunge kuwa raia wa Msumbiji waliotafuta hifadhi nchi jirani ni pamoja na wa maeneo ya Niassa, Nampula, Zambézia, Sofala na Inhambane.
Serikali ilikuwa imetenga kitengo chake cha kutoa msaada wa dharura kwa raia hao.
