Julian Assange anyang'anywa uraia wa Ecuador


Mahakama moja ya Ecuador imemfutia uraia wa nchi hiyo mwasisi wa mtandao wa WikiLeaks Julian Assange. Gazeti la El Comercio limeripoti kwa kunukuu maelezo ya mahakama ya mjini Quito, kwamba yalifanyika makosa wakati mwasisi huyo wa Wiki Leaks mzaliwa wa Austarlia alipopewa uraia wa Ecuador mnamo mwaka 2017.
 
 Assange bado anashikiliwa katika jela yenye usalama mkubwa ya Belmarsh mjini London huko Uingereza. Marekani inataka ikabidhiwe mfichua siri huyo. Assange amekuwa akikabiliwa na tuhuma za kushirikiana na jaasusi wakijeshi wa zamani wa Marekani Chelsea Manning kuvujisha mnamo mwaka 2010, taarifa za ndani za siri kuhusu shughuli za vikosi washirika wa Marekani nchini Afghanistan. 
 
Jumla ya mashtaka 18 yamefunguliwa na Marekani dhidi yake.Akikutwa na hatia anaweza kukabiliwa na kifungo cha miaka 175 jela nchini Marekani. Assange akimbilia katika ubalozi wa Ecuador mjini London mwaka 2012 kupuka kusafirishwa Marekani na alipewa hifadhi katika ubalozi huo na baade kupewa uraia.

 

Chapisha Maoni

Mpya zaidi Nzee zaidi

Popular Items