Al Shabaab watoa somo kwa abiria kwenye basi linaloelekea Mandera

Kundi la watu wanaoshukiwa kuwa wanamgambo wa al-Shabaab walitoa mhadhara wa saa mbili kwa abiria waliokuwa kwenye basi lililokuwa likielekea Mandera katika Mkoa wa Kaskazini Mashariki mwa Kenya, kulingana na ripoti za vyombo vya habari vya Kenya zikiwanukuu polisi.

Polisi walisema wanamgambo wa al-Shabaab waliokuwa na silaha nzito walisimamisha basi la Al Mukaram kati ya Dabacity na Dimu Hill na kuamuru abiria kushuka.

Walitumia zaidi ya saa mbili kutafuta watu kutoka nje ya basi kama ilivyoripotiwa na Daily Nation.

Gazeti hilo pia liliripoti kuwa kundi lililosimamisha basi hilo lilikuwa limegawanyika katika makundi mawili, ambapo baadhi yao walizungumza na abiria hao kwa lugha ya Kisomali huku wengine wakienda porini kujikinga.

 

Post a Comment

0 Comments