Korea Kaskazini yasema haijawahi kuiuzia Urusi silaha na haina mpango wa kufanya hivyo katika siku zijazo, kufuatia ripoti za Marekani kwamba Moscow ilikuwa ikigeukia Pyongyang ili kujaza akiba yao ya silaha.
Maafisa wa Marekani walisema hapo awali kwamba Urusi inaweza kununua roketi na makombora ya mizinga kutoka Korea Kaskazini.
Walisema hatua hizo, pamoja na madai ya ununuzi wa silaha za Iran, zinaonyesha vikwazo vya Magharibi vinazuia juhudi za Urusi katika vita vya Ukraine.
Hata hivyo, Moscow ilikanusha ripoti hizo wakati huo.
Harakati zozote za silaha kati ya nchi hizo mbili zitakuwa zinakiuka vikwazo vya Umoja wa Mataifa.
Siku ya Alhamisi, katika taarifa iliyotolewa na vyombo vya habari vya serikali ya Korea Kaskazini KCNA, afisa ambaye hakutajwa jina katika wizara ya ulinzi ya Korea Kaskazini alisema: ‘’Hatujawahi kusafirisha silaha au risasi kwa Urusi hapo awali na hatutapanga kuziuza.’’
Ilishutumu Marekani, na ‘’vikosi vingine vya uhasama’’, kwa kueneza uvumi ‘’kutekeleza malengo yake ya kisiasa na kijeshi’’.
Mapema Septemba, msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Marekani alisema ununuzi wa Urusi wa Korea Kaskazini ‘’unaweza kujumuisha mamilioni ya roketi na makombora ya mizinga.’’
Lakini msemaji wa Baraza la Usalama la Taifa John Kirby baadaye alionekana kupuuza kauli hiyo, kwa kusema ununuzi ulikuwa bado haujakamilika na hakuna ushahidi wa kupendekeza silaha hizo zingetumika katika vita vya Ukraine.
Uvamizi wa Urusi nchini Ukraine mwezi Februari umethibitisha gharama kubwa kwa jeshi lake, licha ya kutumia silaha za hali ya juu kama vile makombora.
Vikosi vya Ukraine, vinavyotumia silaha za nchi za Magharibi ambazo vimeingizwa nchini humo katika miezi ya hivi karibuni, vimesababisha hasara kubwa.
Silaha nyingi za Korea Kaskazini zilizoundwa na Urusi zilitoka enzi ya Usovieti, lakini ina makombora yanayofanana na yale ya Urusi.
Mnamo Julai, Korea Kaskazini ilikuwa moja ya nchi chache ambazo zilitambua rasmi maeneo mawili ya kujitenga yanayoungwa mkono na Urusi mashariki mwa Ukraine.
Katika kulipiza kisasi, Ukraine ilikata uhusiano wote wa kidiplomasia na Pyongyang.
Mapema mwezi huu, rais wa Urusi Vladimir Putin aliapa kupanua ‘’uhusiano wao wenye tija’’ katika barua kwa mwenzake Kim Jong-un.
0 Comments