F Wananchama wa CCM watakiwa kuvunja makundi ili kupata ushindi wa kishindo | Muungwana BLOG

Wananchama wa CCM watakiwa kuvunja makundi ili kupata ushindi wa kishindo


Mwenyekiti wa Chama cha mapinduzi Mkoa wa Tanga Ustad.Rajab Abdlrahman  amewataka  wanachama na wagombea waliopita kwenye kura za Maoni kuacha makundi baada ya  mchakato kupita kwani umoja ndio utakaoweza kuwapatia ushindi wa kishindo .

Hayo aliyasema wakati wa mkutano mkuu maalumu wa kutafuta kura za wagombea udiwani ,Wabunge na Rais Samia kuputia  Chama cha mapinduzi  hivyo hukuna sababu ya kujenga tofauti  badala yake kuacha makundi kuendelea kutafua kura ili kupata ushindi wa kishindo.

Aidha aliongeza kusema kuwa waliokisaliti Chama wanapaswa kujua Chama  Chama cha mapinduzi kinamsimamo hivyo ni kimeamua kushirikiana pamoja lengo kuu ikiwa kuongeza kwa idadi ya kura ndani ya mkoa wa Tanga.

 Sambamba  na hayo alito wito kwa wale wlioteuliwa kwenye nafasi ya kugombea ubunge au udiwani waache mara moja tambia ya kujitamba mbele ya wale wasioteuliwa ili kuacha kutengeneza makundi vivyohivyo na wale wasioteuliwa wanapaswa kuwa wavumilivu lakini pia kufucha hisia  zao ili Chama kisigawanyike.

Kwa upande wake mzee Musa Shekimweri ambaye alikuwa mwenyekiti mstaafu wa CCM Mkoa aliwataka wajumbe kuweza kutambua kuwa nafasi ya uchaguzi ni moja tu mtu anapoachwa kwenye kura au kutokueuliwa ni kwaida wala sio jambo la kutengenza  chuki na kipindi cha kura za maoni makundi pia kawaida ila baada ya hapo wanapaswa kukaa pamoja na kujenga  nyumba moja.

Alisema cha kufahamu ni kwamba wagombea wanaweza kujitokeza wengi kwenye kiti Kimoja lakini baada ya hapo  atakayekaa kwenye kiti ni mtu mmoja ambaye ndio atakayebahatika tu hivyo hakuna haja ya kugawanyika ndani ya Chama Cha mapinduzi. 

Hata hivyo alitoa ombi kwa viongozi wa CCM kuwa wakati wa Uchaguzi  tarehe 29 mwezi October  wale wazee wote ambao hawezi kutembea na ni wapiga kura wafuatwe majumbani ila wafike kwenye vituo vya wapiga kura wapige kura zao kuwachagua viongozi wao.

Post a Comment

0 Comments