Kwenye maisha unaweza ukawa na undugu na mtu fulani bila wewe kujua kama mtu huyo ni ndugu yako. Hii imetokea kwa wanamuziki wawili Ay na Nay wa Mitego ambao walikuwa ni ndugu ila hawakulitambua hilo.
Nay amesema kuwa wakati wanafanya Remix ya muda wetu ndipo AY alipomuuliza yeye ni mtu wa Mbeya sehemu gani na baadaye wakagundua kuwa wao ni ndugu wa damu kabisa.
"Kiukweli kabisa tulikuwa hatujuani kama mimi na AY ni ndugu fo real kabisa, kuna siku tulikuwa tunafanya remix ya muda wetu ambayo kwenye ngoma hiyo kuna Brother AY, kuna Billnas na Godzillah, unajua AY ni bro mtu wa Mbeya na pia ni mtu ambaye alishawahi nipa nafasi ya kunisikiliza kabla sijatoboa," amesema Nay XXL ya Clouds FM.
"Familia ya mama baada ya kumuelezea kumbe ndugu zake ni ndugu zangu, nikajaribu kumpigia sister wake fulani anamfahamu na mama angu pia tukagundua kuwa mimi na AY ni ndugu yangu wa damu."
Ikumbukwe kwamba AY (Ambwene Yesaya) ni mtu wa Mbeya ambapo mama wa msanii Nay anatokea mkoa huo.