Makamu wa Rais azindua maonyesho ya Nanenane Simiyu


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akizindua Jengo la Kituo cha Elimu kwa Wakulima Kanda ya Ziwa Mashariki wakati wa Uzinduzi wa Sikukuu ya Wakulima Nanenane iliyofanyika leo Kitaifa katika Viwanja vya Nyakabindi Mkoani Simiyu. ambapo ujumbe wa mwaka huu Nanenane kwa maendeleo ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi Chagua Kiongozi Bora 2020.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akiangalia baadhi ya Mazao ya aina mbalimbali ikiwemo Vitunguu maji, Nyanya na Viazi Mviringo alipotembelea mabanda maonesho katika Viwanja vya Maonesho ya Nanenane vya Nyakabindi Mkoani Simiyu.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akiangalia mazalio ya Samaki alipotembelea Banda ya JKT katika Viwanja vya Maonesho ya Nanenane vya Nyakabindi Mkoani Simiyu leo.