PICHA: Mambo yalivyo ndani ya Uwanja wa Nelson Mandela fainali ya ASFC leo

 Ndani ya Uwanja wa Nelson Mandela mashabiki wakisubiri kutazama fainali ya ASFC kati ya Simba dhidi ya Namungo FC mchezo utakaoanza majira ya saa 9:00 alasiri.

Mchezo wa leo ambao ni wa fainali unatarajiwa kuwa na ushindani mkubwa huku ukiwa umebeba hisia kubwa kwa mashabiki pamoja na timu zote kujipanga kuhitaji ushindi.

Tayari mashabiki wameanza kujitokeza kwa wingi ndani ya uwanja ili kushuhudia fainali ambayo ni ya kwanza kufanyika kwenye Uwanja wa Nelson Mandela siku ya leo.