TAKUKURU Mkoa wa Pwani yafanikiwa kuokoa zaidi ya milioni200 kutoka kwa wanyonge


VICTOR MASANGU, PWANI

Taasisi ya kuzuia na kupamba na rushwa Tanzania (TAKUKURU)  Mkoa wa Pwani imefanikiwa kuokoa mali na kiasi cha zaidi ya  shilingi milioni mia mbili katika kipindi cha robo ya tatu  kuanzia  mwezi wa Julai mpaka Septemba  mwaka 2020 kutokana na kushughulikia malalamiko mbali mbali yaliyofanyiwa uchunguzi na kazi.

Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake Mkuu wa Takukuru Mkoa wa Pwani Suzan Raymond alisema kwamba ofisi yake katika kipindi hiki cha robo ya tatu ilipokea malalamiko 318 ambayo kati ya hayo malalamiko 157 unaendelea kufanyiwa kazi katika hatua mbali mbali na malalamiko 74 yalionekana kuangukia katika sheria nyinginezo.

Mkuu huyo alisema kwamba katika kipindi hicho jumla ya kesi 10 zilitolewa hukumu na upande wa wa jamhuri ulifanikiwa kushinda kesi zipatazo 6 kwa washitakiwa kuamuliwa kufungwa jela na wengine kuamuliwa kulipia faini ambapo kesi nne watuhumiwa  hawakukutwa na hatia na hivyo waliweza kuachiwa huru.

Pia Mkuu huyo akizungumzia kuhusiana na halmashauri ya Chalinze iliweza kufanikiwa kurejesha kiasi cha  zaidi ya shilingi milioni 6 ambazo zilitokana na ukiukwaji wa taratibu za mikopo ambayo inatolewa kwa vikundi vya wanawake vijana pamoja na makundi ya watu wenye ulemavu uliofanywa na kikundi cha Miono Saccos kilichopo kata ya miono.

“Katika uchukuzi wetu ambao tulioufanya sisi kama takukuru Mkoa wa Pwani tulibaini kamba viongozi wa kikundi hicho cha miono Saccos yaani Mwenyekiti na katibu wake walipokea mkopo usio kuwa na riba kutoka kwa halmashauri ya chalinze na wao kuamua kwenda kukopesha kwa wafanyabiashara pasipo hata kuwajulisha wahusika ambao ni wana vikundi,”alisema Suzana.

Kadhalika akifafanua kuhusiana na mafanikio ambayo iliyapata ofisi ya Takukuru Kibaha iliweza kufanikiwa kurejesha nyumba ya iliyokuwa ikimilikiwa na Bi. Mayasa Ally iliyokuwa ikishikiliwa na kutaka kuuzwa na Godlisten Ndimbo kinyume kabisa na sheria na taratibu kutoka na madai ya kushindwa kumaliza deni alilokuwa akidaiwa.

Akizungumza zaidi kuhusiana na Ofisi ya Takukuru Wilaya ya Mafia yenyewe katika kipindi hicho iliweza kuokoa kiasi cha  zaidi ya shilingi milioni 4 ambazo zilikusudiwa kuchepushwa na baadhi ya watumishi na mawakala ambao wanafanya kazi katika halmashauri ya Mafia ambao wana dhamana ya kukusanya ushuru kwa kutumia mashine ya kieletroniki.

Pia Suzan alifafanua kuwa katika Wilaya ya Kibiti waliweza kuokoa bati zipatazo 168 zenye thamani ya kiasi cha  zaidi ya shilingi milioni 4 zilizotakiwa kuezekwa katika madarasa ya shule ya msingi Nyambagala iliyopo kata ya Dimani Wilayani Kibiti ambapo awali ilibainika kuwa mkataba huo wa ujenzi wa madarasa hayo kuezeka  mabati ya ukumbwa wa gaige 28 kinyume na makubaliano.

Akifafanua zaidi Mkuu huyo wa Takukuru alieleza kwamba katika Wilaya ya Kibiti waliweza kupambana vilivyo na kufanikiwa kuokoa kisi cha shilingi milioni mbili na nusu kutokana na tozo mbali mbali za kodi kutoka kwa wafanyabiashara wa zao la misitu kwa kuvuna magogo ya miti aina ya mkuruti katika maeneao yasiyoruhusiwa.

Katika hatua nyingine alisema kuwa kwa upande wa Wilaya ya Kisarawe waliweza kumsaidia mwananchi mmoja aliyejulikana kwa jina la Khadija Bani mkazi wa mtaa wa Bomani kulipwa kiais cha shilingi 12 na laki tano kutokana na kuchukuliwa shamba lake na kmapuni ya Rak Kaolinic Limited.

Kwa upande wa Wilaya ya Mkuranga Takukuru iliweza kufanikiwa kuwarejeshea  wakulima wa chama cha msingi cha Kimanzichana kusini kiasi cha  zaidi ya shilingi milioni 34 ambazo walikuwa wamedhulimiwa na viongozi wa bodi ya Amcos na kampuni ya Cofee Traders.

Post a Comment

0 Comments