Wavuvi 8 wafariki baada ya mashua kuzamishwa kwa dhoruba kali Somalia


Wavuvi 8 wameripotiwa kupoteza maisha baada ya mashua kuzamishwa kwa dhoruba kali za mawimbi nchini Somalia.

Wavuvi hao waliozama na kufariki wamebainishwa kuwa raia wa Yemen.

Dhoruba kali ya mawimbi ilitokea hapo jana nyakati za usiku na kuathiri maeneo ya Bosaso na Hafun yaliyoko mkoani Puntland. 

Mvua nyingi zilizonyesha na upepo mkali uliopiga pia uliharibu nyumba na barabara za maeneo hayo.

Post a Comment

0 Comments