https://monetag.com/?ref_id=TTIb Meseji nzuri za kumtumia mpenzi wako ili azidi kukupenda zaidi | Muungwana BLOG

Meseji nzuri za kumtumia mpenzi wako ili azidi kukupenda zaidi

 



  1. Wewe ni kila kitu kwangu.
  2. Nitateseka bila wewe.
  3. Ninataka nikwambie tu kuwa ninakuwaza muda wote.
  4. Ninatamani kuwa mikononi mwako muda wote.
  5. Ninakupenda zaidi ya unavyofikiria.
  6. Unafanya mapigo ya moyo wangu yaende mbio nikikuona.
  7. Najisikia vizuri mno nikikuwaza mpenzi.
  8. Ninajihisi salama nikiwa nawe.
  9. Nikiwa mikononi mwako ninajihisi nimefika!
  10. Ulishaubeba moyo wangu na sitaki uurudishe.
  11. Siwezi kuishi bila wewe mpenzi.
  12. Sitosahau usiku ule ambao tuli.
  13. Tabasamu lako linanipoteza kabisa.
  14. Unanistaajabisha kila siku.
  15. Nitafanya lolote ili niwe nawe.
  16. Ninakutamani kila saa.
  17. Ninaona fahari kuwa na wewe. 
  18. Wewe ni wangu daima na milele.
  19. Unanifaa sana mpenzi.
  20. Sijui ningekuwa wapi bila wewe.
  21. Kila siku tunapokuwa pamoja naona ninaishi ndoto yangu ya siku nyingi.
  22. Moyo wangu unasisimka ninapokuwa nawe.
  23. Hakuna mtu aliyewahi kuwa karibu nami na akanifanya nijisikie raha kama unavyonifanya nijisikie.
  24. Ninahesabu muda mpaka pale nitakapo pata busu lako tamu.
  25. Ni kama vile uliumbwa kwa ajili yangu.
  26. Wewe ni mtu pekee ambaye siko tayari kukuacha. 
  27. Kila saa wewe ndiye chaguo langu.
  28. Unanifanya nijiamini sana mpenzi.
  29. Wewe ndiye baraka kubwa niliyowahi kuipata.
  30. Wewe ni mzuri sana aisee.
  31. Nikikuwaza tu, hata niwe na siku mbaya, itageuka kuwa nzuri tu
  32. Moyo wangu unakuhitaji sana sasa.
  33. Ninatamani ungekuwepo hapa na mimi.
  34. Ninavyokupenda jamani, acha tu!
  35. Ninajihisi mwenye bahati sana kukupata wewe kama rafiki wa karibu na mpenzi pia.
  36. Hata milele hainitoshi kuwa na wewe.
  37. Natamani ungekuwepo hapa ukanishika mkono na ukanivuta kwako.
  38. Nimekuwaza siku nzima. Ahsante kwa usiku mzuri kama ule.
  39. Sikuwahi kujua kuwa unaweza kummiss mtu hata kabla hajaondoka, mpaka nilipokujua wewe ndio nikaamini.
  40. Maisha yetu pamoja ni tafsiri ya upendo.
  41. Natumai uko na siku njema, mwenzio nashindwa kuacha kukuwaza muda wote.
  42. Daima hujawahi shindwa kunifanya nitabasamu wakati wote.
  43. Najikuta nikishindwa kujizuia kutabasamu kila ninapofikiria kukuona ukirudi toka kazini.
  44. Wewe ni wangu, kipenzi cha nafsi yangu.
  45. Ninakuthamini sana mpenzi.
  46. Unanifanya nijisikie mwenye bahati sana kuliko wote.
  47. Natamani nikupe mabusu mazito kila ninapokuona.
  48. Nataka niamke pembeni yako siku zote za maisha yangu.
  49. Wewe ni mcheshi sana, unanifanya niwe mwenye furaha wakati wote.
  50. Ninashukuru sana nimekujua.

Post a Comment

0 Comments