Asilimia kubwa ya Waisrael yawachukia Wapalestina


Kulingana na utafiti wa maoni uliofanywa huko Israel, vijana wengi wa Kiyahudi huwachukia Wapalestina ambao ni raia wa Israel na hupendelea kwamba Wapalestina hao wanyakuliwe uraia wa Israel.

Chuo Kikuu cha Waebrania cha Jerusalem, kilichoko Mashariki mwa Jerusalem, kilionyesha matokeo ya utafiti wa maoni ya umma wa vijana 1,100 wenye umri wa miaka 16 hadi 18.

Kulingana na utafiti uliofanywa mnamo Mei-Julai mwaka jana, katika asilimia 66 ya vijana wa Kiyahudi wa Kiothodoksi waliofanyiwa utafiti, asilimia 42 ya Wayahudi wenye dini, na asilimia 24 ya wayahudi wasio na dini wanawachukia Wapalestina, walio raia wa Israel.

Wapalestina wa Israel walio na idadi ya zaidi ya milioni 1.9 huchangia karibu asilimia 21 ya idadi ya watu wote nchini Israel.

Wapalestina wa Israel wanawakilishwa na manaibu 15 tu katika bunge lenye viti 120.


 

Post a Comment

0 Comments