Familia ya kijana aliyefariki yafungua kesi ya dola milioni 100 dhidi ya kampuni ya umeme nchini Marekani


Familia ya Cristian Pineda mwenye umri wa miaka 11, ambaye aliripotiwa kufariki kwa ugonjwa wa baridi kazi wa hypothermia katika jimbo la Texas nchini Marekani (USA), ilifungua kesi ya dola milioni 100 dhidi ya kampuni ya umeme kwa tuhuma za uzembe mkubwa.

Baridi kali ilizuka bado inaendelea kusababisha vifo vya watu nchini Marekani.

Katika jimbo la Texas ambalo lilikumbwa na ukatizaji wa umeme na ukosefu wa joto la kutosha, Cristian Pineda mwenye miaka 11 alifariki wiki iliyopita.

Wataalam wa Autopsy waliripoti kwamba Cristian alifariki kutokana na hypothermia.

Familia ya kijana huyo iliishtaki kampuni ya umeme kwa kesi ya dola milioni 100 kwa mashtaka ya "uzembe mkubwa."

Ongezeka la sumu ya karbon monoksidi na hypothermia kutokana na matumizi ya jenereta nchini humo limezua hofu kutokana na kesi za athari zinazozidi.


Post a Comment

0 Comments