https://monetag.com/?ref_id=TTIb Mkojo wa wajawazito biashara mpya Dar | Muungwana BLOG

Mkojo wa wajawazito biashara mpya Dar

 


Dar es Salaam. Unaweza kusema mkojo wa wajawazito umegeuka ‘dili’ baada ya Kampuni ya Polai (Tz) CO LTD kuinunua kwa maelezo kuwa ni tiba ya magonjwa ya binadamu.


Uchunguzi uliofanywa na gazeti hili kwa siku 14 umebaini kuwa ukusanyaji wa mikojo hiyo unafanyika kwa usiri mkubwa mkoani hapa, kwa wajawazito ambao hufuatwa majumbani na kushawishiwa kukubali.


Mikojo hiyo hukusanywa na huwekwa kwenye vikopo kisha kupelekwa kwenye nyumba iliyopo Mtaa wa Mferejini Kata ya Manzese, kabla ya kupelekwa kwa raia wa kigeni anayetajwa kuwa mmiliki wa kampuni hiyo.

Post a Comment

0 Comments