Tetesi za soka kimataifa


 Rais wa Barcelona Toni Freixa anaamini itawezekana kuwasajili washambuliaji wa PSG na Ufaransa Kylian Mbappe, 22, na mwenzake wa Borussia Dortmund na Norway Erling Braut Haaland, 20. (Marca)

Barcelona imeongeza hamu yake katika kumsajili mshambuliaji wa Sweden na Real Alexander Isak, 21, huku wakiwa na mpango wa kumsajili mshambuliaji mpya mwisho wa msimu huu. (ESPN)

Kipa wa England Dean Henderson, 23, atajaribu kuondoka Manchester United mwisho wa msimu huu iwapo hatoshirikishwa katika kikosi cha kwanza cha timu hiyo msimu ujao.. (Manchester Evening News

Tottenham Hotspur huenda ikamuajiri mkufunzi wa klabu ya RB Leipzig Julian Nagelsmann kuchukua nafasi ya mkufunzi wake Jose Mourinho. (Telegraph - subscription required)

Juventus na Inter Milan zimejiunga katika kinyanganyiro cha kumsajili mshambuliaji wa Manchester City, 32 raia wa Argentina Sergio Aguero, ambaye tayari amezungumza na Barcelona na Atletico Madrid kuhusu uwezekano kuhamia katika klabu hizo mwisho wa msimu huu. (Sun)

Manchester United imekataa kuruhusu kifungu kitakachoiruhusu West Ham kumsaini kiungo wa kati wa West Ham Jesse Lingard, 28 kwa dau fulani mwisho wa msimu huu. (Times - subscription required)

Barcelona imeongeza hamu yake katika kumsajili mshambuliaji wa Sweden na Real Alexander Isak, 21, huku wakiwa na mpango wa kumsajili mshambuliaji mpya mwisho wa msimu huu. (ESPN)

Beki wa Jamhuri ya Ireland Matt Doherty anakabiliwa na switofahamu kuhusu hatma yake katika klabu ya Tottenham huku mkufunzi Jose Mourinho akiondoa wasiwasi kuhusu mchezaji huyo kuendelea kutoa huduma zake katika klabu hiyo.. (ESPN)

RB Leipzig inajiandaa kumuuza mchezaji anayelengwa na Tottenham Marcel Sabitzer, kiungo huyo wa kati wa Austria mwenye umri wa miaka 26, na wanatafuta mchezaji atakayechukua yake nafasi mwisho wa msimu huu. (Football Insider)

Mkufunzi wa Chelsea Thomas Tuchel amekiri kujaribu kumsajili mshambuliaji wa Uruguay Luis Suarez, 34, wakati alipokuwa akiiongoza PSG , lakini hafikirii kumsajili mshambuliaji huyo wa zamani wa Liverpool katika uwanja wa Stamford Bridge. (London Evening Standard)

Post a Comment

0 Comments