Balozi wa Italia Nchini DRC, Luca Attanasio aliuawa katika shambulio Februari 22. Serikali imewashutumu waasi wa FDLR wenye asili ya Rwanda kwa shambulio hilo
Balozi Attanasio alikuwa katika msafara wa Shirika la mpango wa Chakula Duniani (WFP) na walishambuliwa karibu na Mji wa Goma, mashariki mwa Congo
Hata hivyo, kundi la FDLR limekanusha kuhusika na shambulizi hilo kwa kile inachosema vikosi vyake viko mbali na eneo la shambulizi
Maafisa katika Mbuga ya Wanyamapori ya Virunga wanasema shambulio hilo lilikuwa jaribio la utekaji nyara lililoshindikana, pale walipoingilia kati mara moja
0 Comments