Biden amuonya Putin katika ziara yake yake kwanza ya kigeni


Rais wa Marekani Joe Biden ameanza safari yake ya kwanza nje ya nchi yake kwa onyo kwa taifa la Urusi

Biden alisema Moscow itakabiliwa na athari mbaya ikiwa itahusika katika "shughuli mbaya".

Biden alithibitisha kuwa atatoa ujumbe wazi kwa Rais wa Urusi Vladimir Putin, katika mahojiano na umati wa wanajeshi wa Amerika na familia zao jana, Jumatano, huko Mildenhall Air Force Base, ambapo ndege yake ilitua kabla ya kuelekea Cornwall, kusini magharibi mwa Uingereza.

Biden alisema: "Hatutafuti mzozo na Urusi.

Tunataka uhusiano thabiti. Ujumbe wangu uko wazi: Marekani itajibu kwa nguvu na kwa uthabiti ikiwa Urusi itajihusisha na shughuli zinazodhuru.

Mnamo Aprili, Putin alishutumu nchi za Magharibi kwa kujaribu "kuiwinda" Urusi, akiwaonya wasivuke "mstari mwekundu’

Katika kila kituo cha safari yake ya kwanza ya kigeni kama rais wa Marekani , Biden ameonekana kutoa ujumbe wa wazi kwamba "Marekani inarudi na nchi za demokrasia ulimwenguni kote zinashirikiana bega kwa bega mbele ya changamoto kubwa zaidi ambazo zinatishia siku zijazo

Post a Comment

0 Comments