Mchopanga afunguka kuhusu elimu yake "Nina degree"

 


Juzi Jumamosi, Juni 19, Rais Samia Suluhu Hassan aliwateua Wakuu wa Wilaya na kutajwa kwa jina la msanii Juma Chikoka maarufu `Mchopanga’ kuwa Mkuu wa Wilaya ya Rorya, kumekuwa na mjadala mkubwa kuhusu elimu yake akilinganishwa na cheo alichopewa.

Kupitia video inayosambaa mtandaoni ambayo alifanyiwa mahojiano na kituo cha CloudsTv, Mchopanga ameeleza ana Shahada ya Masuala ya Sanaa, elimu aliyoichukulia Chuo Kikuu cha Bangalore nchini India.

Mteule huyo ameeleza kuwa, aliipata elimu yake ya Sekondari katika Shule ya Kinondoni na baada ya hapo akachaguliwa kuendelea kidato cha tano Shule ya Sekondari Tambaza

Post a Comment

0 Comments