Mlipuko wa Somalia waua zaidi ya wanajeshi 10


Zaidi ya wanajeshi 10 wameuawa baada ya mlipuaji wa kujitoa mhanga kujilipua katika kambi moja ya kijeshi iliyopo mkuu wa Somalia, Mogadishu, ripoti zinasema.

Mwanahabari aliyekua katika eneo la tukio amesema mlipuaji huyo alijidai kuwa mwanajeshi, na kuingia katika kambi ya jeshi ya Wadajir na kuanza kulipua vilipuzi alivyokuwa amejifunga kiunoni, wakati wa mafunzo ya asubuhi.

Watu wengine 10 pia wamejeruhiwa.

Post a Comment

0 Comments