Upendo unahitaji mambo haya

 

Upendo unahitaji mambo yafuatayo ambayo ndio msingi wa upendo. Kuna vitu ambavyo upendo unahitaji;

1. Tumaini (Hope)
Upendo unahitaji Tumaini, kwa lugha ya Kiyunani ‘elpis’ lenye maana ya
(a) Favourable
(b) Confident, expectation

2. Uvumilivu (patience)
Upendo unahitaji uvumilivu kuvumiliana. Hakuna mwanadamu aliyekamilika katika mambo yote, unajua Waswahili wanasema “mvumilivu hula mbivu “ mvumilivu katika upendo maana yake hii ni shule ya kila siku, tunajifunza kutokana na makosa. Uvumilivu unatakiwa sana katika upendo - unajua kumfanya mwenzi wako kuwa kama wewe unavyotaka awe inahitaji uvumilivu. Hilo ni kweli, maana mmetoka mazingira tofauti na malezi tofauti; hivyo kumbadilisha inahitaji uvumilivu.

3. Kiasi
Kiasi ni kitu muhimu. Chochote kinachofinywa zaidi ni hatari, unatakiwa uwe na kiasi katika mambo yako ili uweze kudumu katika upendo maana upendo unahitaji kiasi. Usijifanye uko (busy) sana unakosa hata nafasi/muda wa kukaa na mwenzi wako, lakini wewe unarudi usiku, huo sio upendo. Nakuombea uwe na kiasi ili uenzi katika maisha yako.

4. Kutiwa moyo
Upendo unahitaji kutiwa moyo. Mtie moyo mwenzi wako ukimwambia pole asali wangu wa moyo, Unafanya vizuri sana, umefanya vizuri sana, unapoweza kumtia moyo mwenzi wako kwa yale anayofanya yanamuhamasisha kutenda zaidi na kukupenda zaidi. Kutiwa moyo ni kufarijiwa, moyo unahitaji kutiwa moyo, kuthaminiwa. Hivyo katika upendo unahitaji kumtia moyo mwenzi wako ili upendo huo udumu maishani mwako. Ikiwa hauna tabia ya kumtia moyo mwenzi wako ipo siku utampoteza, akipata watu wanaothamini mambo anayoyafanya na kumfariji. Atulie badilika uuteke upendo kwa kufuata masharti yake.

5. Kutambuliwa
Upendo unahitaji kutambuliwa katika maisha yako na kujua umuhimu wake. Kutambuliwa ni kitu muhimu sana katika maisha, kumtambua mpenzi wako na umuhimu wake kwako. Atambulike toka moyoni mwako kuwa anafaa kuwa mumeo au mke wako, hivyo upendo unahitaji sana utambuliwe na wewe mwenyewe. Umfahamu na umuelewe kiundani.

6. Uaminifu
Upendo unahitaji uaminifu kwa mwenzio sio msaliti wenye kujitunza na kujiheshimu mtu asiye na hila ndani yake uaminifu ni dawa ya upendo katika maisha yetu tukikosa uaminifu sisi kwa sisi upendo hautaweza kukaa pamoja nasi.

7. Usawa
Upendo unahitaji usawa unajua mapenzi ni kusaidiana hakuna kiongozi wa mapenzi bali tunasaidiana hivyo huo ndio usawa katika mapenzi upendo unahitaji usawa huo wewe unawajibu kwa mwenzi wako na mwenzi wako anawajibu kwako.

8. Urafiki
Upendo unahitaji urafiki upendo hujenga urafiki mwenzi wako ni rafiki yako kuliko marafiki ulionao katika maisha yako- Mapenzi wako sio adui yako mficha siri wako usimuogope maana upendo hauna hofu unatakiwa kuzungumza na rafiki yako kirafiki ili upendo uwezo kudumu na kushamili.

9. Kukubalika
Upendo unahitaji kukubalika, kupokelewa toka moyoni mkubali mwenzi wako apate kibali moyoni na maishani mwako ukimkubali hautamuumiza hivyo upendo unataka kukubalika hapo utafurahia maisha yako.

10. Ukweli
Upendo unahitaji ukweli,upendo ni adui wa uongo unatakiwa uwe mkweli katika mapenzi yenu,ukweli hujenga upendo, ukweli huimarisha mahusiano,upendo unahitaji mtu ambaye ni mkweli kwa mwenzi wake,ukweli ndio upendo wenyewe unatakiwa uwe mkweli ili upendo uchukue nafasi moyoni mwako.

11. Imani
Upendo unahitaji imani na imani ni kuwa na uhakika wa mambo yatarajiwayo ,ni bayana ya mambo yasio onekana. Unatakiwa kuwa na imani na mwenzi wako, imani katika mahusiano ni muhimu sana kuaminiana ,toa wasiwasi kwa mwenzi wako, mwamini kuwa amekuchagua wewe na hakuna mwinginen wewe uko peke yako.

12. Penzi
Upendo unahitaji penzi la kweli linalotoka moyoni ,penzi kwa mpenzi wako ni muhimu sana kama litatumika kwa utaratibu na kwa uaminifu kabisa maana penzi linahitaji muda hivyo hivyo unatakiwa uwe na muda wa kutosha ili uweze kupata pendo la kweli.

13. Ujasiri
Upendo unahitaji uwe jasiri katika hali zote ujasiri katika kunena ,ujasiri kutenda, ujasiri katika kuuzungumzia upendo kwa mwenzi wako upendo unamhitaji mtu jasiri sio kitu rahisi kama wengine wanavyozungumzia.

14. Mawasiliano
Upendo unahitaji mawasiliano maana mawasiliano hutengeneza mahusiano ,bila mawasiliano hakuna mahusiano imara na ili ujenge msingi mzuri wa mahusiano yako unahitaji uwe mtu mzuri katika mawasiliano- mawasiliano yana uwezo mkubwa sana wa kutunza mahusiano hivyo upendo unahitaji mawasiliano.

15. Asante
Upendo unahitaji neno asante kwa mwenzi wako kwa lolote atakalo litenda kwako kama atakupa zawadi asante hasa kwa mpenzi wako ni neno muhimu sana na linaongeza nguvu ya mapendo
Uwe unatumia neno hili asante kwa mpenzi wako maana upendo unahitaji neno hili ASANTE.
Hata baada ya kutoka katika tendo la ndoa sema asante maana ni tendo la ndoa ni matokeo ya mapendo. Hivyo upendo unahitaji ASANTE.

16. Haki
Upendo unahitaji haki ,unatakiwa umtendee haki mwenzi wako usimyime haki yake ya msingi kumtunza kumpenda na kumtimizia haki zake zote, najua unajua haki za mpenzi wako- upendo ili ukomae unahitaji haki iwepo katika mahusiano yenu.

17. Sifa
Upendo unahitaji sifa ,unatakiwa kumsifia mwenzi wako kuwa umependeza sana mpenzi wangu, unapika vizuri kuliko wengine, mpenzi wangu umevaa vizuri, unavutia mpenzi wangu, umeumbika vizuri, unatabasamu zuri , kwakila anachokifanya kizuri kwako msifu usiache wengine wamsifu mume wako au mke wako utampoteza maana sifa inanguvu sana katika kuimarisha upendo.

18. Upole
Upendo unahitaji upole ,upendo hauwezi kudumu katika ukali, upendo unajengwa na upole maana upole hujenga lakini hasira hubomo,uwe mpole unapozungumza na mwenzi wako upole hugeuza hasira kuwa furaha.

Hivyo ili ufanikiwe katika kutunza mahusiano yenu unatakiwa uwe mpole hata kama umesikia kitu kibaya kwa mwenzi wako unatakiwa uwe mpole ili uweze kufanikiwa kujua unachotaka kujua ,Upole ni mlezi wa upendo.

19. Kutetea (Defending)
Upendo unahitaji utetezi, Unajua unavyoamua kumpenda mtu unatakiwa umtetee unapoona ananenewa mabaya, usichangie kunena mabaya juu ya mpenzi wako usimchafue mpenzi wako, hatua uliyofanya kumpenda tayari umefanyika mtetezi wa mpenzi wako, usikubali dada, mama, baba, mjomba,na marafiki zako wanamnena mabaya mpenzi wako mtotoe kwa bidii ficha aibu ya mwenzi wako .

Ukitaka Upendo usiharibike na uimarike unatakiwa uwe mtetezi mzuri kwa mwenzi wako. Hivyo upendo unahitaji mtetezi.

20. Kutoshelezwa (satisfication)
Upendo unahitaji kutosheleza, upendo hauhitaji kulipuliwa, unahitaji utoshelezwe, unatakiwa kumtosheleza mwenzi wako sawa sawa, usiwe kama kuku upendo hauhitaji kilipuliwa unahitaji kutoshelezwa.

21. Furahi (Enjoyment)
Upendo unahitaji furaha ,unatakiwa umfurahishe mpenzi wako kwa kila kitu ,mfanye afurahi na kufurahia upendo wako unaompa.

22. Hisia (Fellings)
Upendo unahitaji hisia, unatakiwa kuonyesha hisia kali za mapenzi kwa mwenzi wako ,unajua kuwa upendo ni hisia kali?

Muonyeshe mpenzi wako hisia kali za mapenzi ulizonazo kwake –maana upendo ili ukuwe unahitaji mtu mwenye hisia za mapenzi.

23. Adabu (Discipline)
Upendo unahitaji adabu, Upendo unamtafuta mtu mwenye adabu, mtiifu, mnyenyekevu upendo unakaa kwa mtu mwenye adabu ukiwa na adabu hutatoka nje ya ndoa yako, hutaweza kumsaliti mumeo wako au mwenzi wako lakini kama humpi anachostahili akitoka kutafuta faraja nje basi jilaumu wewe maana nae anataka furaha.

24. Kujali (Caring)
Upendo unahitaji kujali, unatakiwa kuonyesha kuwa unajari kwa mpenzi wako,unamjari,muonyeshe kuwa unamjari,Unamheshimu,unamdhamini hauko tayari kumpoteza mteende mema mwenzi wako,ukijali utatunza upendo wako usipotee-mpendezeshe mwenzi wako,mfanye aingie mtaani,n.k. akilinga cheka pamoja naye, lia pamoja naye.

25. Kupenda (Love)
Upendo unahitaji kupendwa unajua unatakiwa kupenda unapopendwa maana upendo unaishi mahali unapopendwa unatakiwa kuonyesha ni jinsi gani unavyompenda.

Upendo wa kweli hauna hofu muonyeshe mapendo mwenzi wako bila hofu na watu watajua jinsi uanvyompenda usiwape maadui nafasi ya kuonyesha upendo wao kwa mwenzi wako.
Mpende mpenzi wako kutoka ndani ya moyo wako maana upendo unahitaji kupendwa.

26. Msamaha (Appologizing/argrivment)
Upendo unahitaji msamaha, msamaha ndio upendo wenyewe rafiki ningependa kukwambia
kuwa unapojua umemkosea mpenzi wako ninakusihi uwe mwepesi kuomba msamaha, hakuna mwanadamu aliyekamilika wote huwa tunakosea ila neno msamaha liwe karibu naomba unisamehe na wewe unayeombwa msamaha unatakiwa uwe na moyo wa kusamehe na ukisamehe hutakiwa kukumbuka tena kama tutakuwa watu wa kuomba msamaha na kutorudi tena waliyofanya na kusamehe na kutokumbuka tena ,msamehe mwenzi wako toka moyoni.

27. Kukumbatia (Hagging)
Upendo unahitaji kukumbatiwa, unajua hapa ni eneo muhimu sana kwa wapendanao,kuna utofauti wa kumkumbatia rafiki,mzazi na mpenzi wako- unapomkumbatia mpenzi wako lazima watu waone utofauti mkubwa na jinsi unavyomkumbatia mpenzi wako unatakiwa umkumbatie vizuri sana hadi utakaposikia mapigo yake ya moyo. Unatakiwa umsogeze karibu sana na wakati yupo kifuani mwako unatakiwa uwe na maneno matamu ukimnong’oneza masikioni mwake yanayowakalisha upendo wako kwake hadi anayekumbatiwa ajue kuwa amependwa na mtu Fulani wala hatakiwi kuona aibu ni mali yako-Hivyo upendo unahitaji kukumbatiwa kama Ishara ya kukubaliwa.

28. Ushauri (advising)
Upendo unahitaji kushauriwa ,mashauri hujenga taifa mashauri hujenga mahusiano.
Unatakiwa uwe mtu mwenye ushauri mzuri kwa mwenzi wako, mshauri unapomuona anaenda kinyume na wewe, mshauri anapokosea, kubali kushauriana na mwenzako, muweke chini na kumshauriana na jinsi mtakavyoweza kuendesha familia yenu.

Mshauriane kabla ya kufanya kitu usiwe mwenye amri kwa mwenzi wako hapana upendo wa kweli umejaa mashauri ili uwe mtu mwenye mafanikio unatakiwa uwe na mshauri mzuri – mshauri wa kwanza kabla ya yote ni mwenzi wako – maana upendo unahitaji ushauri ukiwa mtu usiyetaka kushauriwa hutaweza kufika mbali.

Nlyumba nzuri na yenye mafanikio imejaa ushauri mzuri na wenye matokeo chanya.

29. Majadiliano (Discussion)
Upendo unahitaji majadiliano ya amani, unajua kuwa majadiliano ya amani ni mazuri sana maana wewe unaweza kuwaza kuuza nyumba kwa sababu ya hasira lakini majadiliano yatakukumbusha wapi umetoka, wapi ulipo na wapi unakwenda ……?

Majadiliano kwa wapendanao ni kitu muhimu sana maana yanaimarisha upendo wenu na yana nguvu ya kuwapeleka katika kiwango kikubwa cha mahusiano yenu, usiwe mtu wa kujiamulia mambo katika familia.

Acha ubinafsi badilika wewe mwenyewe huwezi kuipeleka familia katika mafanikio kama una wadharau wa nyumbani mwako.

Hivyo upendo ili udumu unahitaji majadiliano.

30. Uwazi (Openly)
Upendo unahitaji uwazi ,unatakiwa uwe muwazi kwa mwenzi wako mwambie kweli nini unataka na nini hutaki, nini ulifanya na kama ulikosea mwambie.

Jaribu kuwa muwazi kwa mwenzi wako, kwa nini unamficha mambo yako, mapenzi ya kweli hayana maficho, kama unapesa Benki mwambie unamficha kwanini, kama ulizaa nje ya ndoa mwambie usimfiche….. Utasababisha matatizo makubwa sana wakati mwenzi wako atakapo tambua kuwa ulimdanganya.

31. Kubembelezwa (Pamper)
Upendo unahitaji kubembelezwa, unatakiwa kumbembeleza Mwenzi wako.

Acha mpenzi wako adeke kwako, na unatakiwa umdekeze mwenzi wako kwa kumpakata, mbemebeleze, muimbie nyimbo nzuri za mapenzi, cheza naye, mbebe mwenzi wako, cheka na mpenzi wako, muache ajiachie kwako, huyo ndiye mwanao wazazi wake wamekukabidhi; umlee na kumtunza, mfute machozi, muogshe, mpake mafuta.

Mabembelezo yanafaa sana kwa mtu na mpenzi wake, deka kwake naye adeke kwako na hapo ndipo upendo utakapodumu katika maisha yenu.
Maana upendo unahitaji kubembelezwa.

32. Kuvuta ukaribu na umakini (Splash)
Upendo unahitaji ukaribu na umakini sana, unatakiwa utengeneze ukaribu na umakini na mwenzi wako asiwe mbali nawe. Jaribu kumsogeza karibu nawe kwa kumuonyesha kuwa upo makini sana na yeye, utaona jinsi upendo utakavyozidi kuongezeka katika maisha yenu.

Upendo wa kweli unahitaji uvute ukaribu na umakini kumsikiliza mwenzi wako, kumtia moyo, kumuelewa anachosema na kutenda hapo upendo hautakimbia katika maisha yenu.

Post a Comment

0 Comments