https://monetag.com/?ref_id=TTIb Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Afrika ya Kati ajiuzulu | Muungwana BLOG

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Afrika ya Kati ajiuzulu

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Afrika ya Kati (CAR) Firmin Ngrebada, amewasilisha ombi la kujiuzulu kwake kwa Rais Faustin Archange Touadera.

Katika ujumbe wake aliotoa kwenye akaunti yake ya Twitter, Ngrebada aliripoti kwamba yeye na baraza lake la mawaziri waliwasilisha ombi la kujiuzulu kwao kwa Rais Touadera.

Ngrebada amekuwa akihudumu kama waziri mkuu wa serikali tangu mwaka 2019.

Rais Touadera anatarajiwa kutangaza baraza jipya la mawaziri hivi karibuni.

 

Post a Comment

0 Comments