ICC yataka msaada wa kifedha wa un kwa minajili ya kuchunguza Libya na Darfur


Mwendesha Mashtaka wa Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu amewasilisha ripoti mpya ya maendeleo kuhusu uchunguzi wake nchini Libya. Mbele ya Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa mjini New York, Karim Khan alitoa wito wa ushirikiano wa nchi wanachama wa baraza hilo.


Mwendesha mashtaka "amekata rufaa" kwa Baraza la Usalama kufadhili uchunguzi wake kuhusu Darfur na Libya. Tofauti na kesi nyingine za ICC, Umoja wa Mataifa ndio ulipeleka mahakamani kesi hizi mbili mwaka wa 2005 na 2011. Lakini hadi sasa, umoja huo haujawahi kukubali kufadhili kesi hizo.


Miezi sita baada ya kuchukuwa hatamu ya uonozi wa Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu, Karim Khan hajatoa tangazo lolote madhubuti. Kwa miaka kumi, Mahakama imechunguza pande zote, bila mafanikio yoyote ya kweli. Hakuna hati yoyote ya kukamatwa, ikiwa ni pamoja na ile iliyomlenga Saif al-Islam Gaddafi, mgombea urais wa mwezi Desemba, iliyowahi kutekelezwa.


Lakini mwendesha mashtaka hachunguzi tu ukandamizaji wa mwaka 2011. Alikuwa akisubiri kwa hamu uhalifu dhidi ya wahamiaji waliofungwa nchini Libya. Saa chache kabla ya ripoti yake, mashirika matatu yasiyo ya kiserikali ikiwemo FIDH yalilaani uhalifu dhidi ya ubinadamu unaofanywa na Walibya dhidi ya wahamiaji. Mashirika hayo matatu pia yameshtumu, lakini kwa tahadhari, sera ya uhamiaji ya Umoja wa Ulaya.


Mjini New York, mwakilishi wa Libya alimtaka mwendesha mashtaka kutowalenga Walibya peke yao kuhusu suala la uhamiaji. "Sote tunajua kwamba biashara haramu ya binadamu na magendo ni uhalifu wa kimataifa," alisema.

Post a Comment

0 Comments