Kina Mbowe wakwama mahakamani

 


Mahakama Kuu Divisheni ya Makosa ya Rushwa na Uhujumu Uchumi imekubali pingamizi la mawakili wa Serikali la kutopokea barua kama kielelezo cha ushahidi wa upande wa utetezi katika kesi ndogo ndani ya kesi kubwa ya ugaidi inayomkabili Mwenyeki wa Chadema, Freeman Mbowe na wenzake watatu.


Uamuzi huo umetolewa leo Jumatatu Novemba 29, 2021 na Jaji Joachim Tiganga na kueleza kuwa mshtakiwa huyo Mohamed Ling'wenya hajaweza kuieleza mahakama ni kwa nini barua hiyo inamhuri wa naibu msajili.


Jaji ameeleza kuwa katika mazingira hayo mahakama imeshindwa kuelewa kama hiyo barua aliyotaka kuitoa ndio hiyo iliyopelekwa kwa RPC.

Post a Comment

0 Comments