Mume amjengea mkewe nyumba kama ya Taj Mahal

 


Mfanyabiashara mwenye umri wa miaka 52 nchini India amejenga mfano mdogo wa Taj Mahal kuwa nyumba ya mke wake wa miaka 27.


Anand Prakash Chouksey amejenga "mnara wa upendo" wake - nyumba ya vyumba vinne inayofanana na ajabu ya usanifu jwa jengola Taj mahal katika jiji la Burhanpur katikati mwa jimbo la India la Madhya Pradesh.


"Ilikuwa zawadi kwa mke wangu lakini pia kwa mji na watu wake," Bw Chouksey aliambia BBC.


Imewekwa ndani kabisa ya mali ya Bw Chouksey - baadhi ya ekari 40-50 za ardhi, ikiwa ni pamoja na hospitali - nyumba hiyo imekuwa ikivutia wageni wengi.



Watu hutembea kwenye nyasi na kupiga picha, alisema. "Watu wengi pia wameanza kupiga picha zao za kabla ya harusi hapa," Bw Chouksey aliongeza.


"Siwazuii kwa sababu katika mji wetu, sisi ni jamii iliyoshikamana kwa karibu ambapo kila mtu anamjua mwingine. Kwa hiyo, nyumba yangu iko wazi kwa wote."


Bw Chouksey alisema kuwa sio wageni wote wanaoruhusiwa kuingia ndani ya nyumba hiyo kwa sababu " ni nyumba yetu na tunaishi humo".


Lakini wakati mwingine, familia huwafurahisha wageni wake wanaokuja na kustaajabia mambo ya ndani ya nyumba hiyo yenye kupendeza - michoro ya maua ambayo hupamba kuta za marumaru na sakafu, na madirisha yake ya kimiani.


Nyumba hiyo ina vyumba viwili vikuu vya kulala ambavyo viko kwenye sakafu mbili tofauti. Pia ina maktaba na chumba cha kutafakari. Chumba cha kuchora huangazia nguzo za marumaru, ngazi zilizopinda na dari iliyopambwa.

Post a Comment

0 Comments