Aliyeteuliwa u-RC na Samia atenguliwa


Rais Samia Suluhu Hassan, ametengua uteuzi wa Dkt. Raphael Chegeni, aliyemteua usiku wa kuamkia Julai 28, 2022, kuwa Mkuu wa mkoa wa Mara, na kumteua Meja Jenerali Suleiman Mzee kuchukua nafasi hiyo.


Taarifa hiyo imetolewa hii leo Julai 31, 2022, na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu, Zuhura Yunus, na kusema Meja Jenerali Mzee, ataapishwa kesho Agosti Mosi, 2022.


Meja Jenerali Suleiman Mzee, alikuwa kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza.

Post a Comment

0 Comments