F RAS Manyara awaaga wachezaji wa SHIMIWI | Muungwana BLOG

RAS Manyara awaaga wachezaji wa SHIMIWI


Na John Walter -Babati
Katibu Tawala wa Mkoa wa Manyara, Maryam Muhaj, amewaaga wachezaji 22 wanaokwenda kushiriki Michezo ya Shirikisho la Michezo ya Wizara na Idara za Serikali (SHIMIWI) jijini Mwanza, ambayo yatafanyika kwa siku 17 mfululizo.

Akizungumza wakati wa kuwaaga, Muhaj aliwapongeza kwa kuchaguliwa kuiwakilisha Manyara na kusisitiza kuwa wanapaswa kuibeba timu hiyo kama alama ya mkoa mzima.

Alisema michezo ni afya, inajenga undugu pamoja na mahusiano mazuri, hivyo wanapaswa kuitumia fursa hiyo kujitangaza vizuri na kuipa heshima Manyara.

"Kauli mbiu ya mwaka huu ni Michezo kwa watumishi kuongeza tija kazini, Jitokeze kushiriki uchaguzi mkuu wa mwaka 2025 kwa amani na utulivu.

Aidha, aliwataka wachezaji kushirikiana na kuonyana endapo mwenzao ataenda kinyume na maelekezo, huku akiwapongeza wakuu wa taasisi kwa kuwaruhusu watumishi kushiriki na kugharamia ushiriki wao katika michezo hiyo.

Kwa upande wake, Mkuu wa msafara wa timu hiyo, Wakili Jackson Kisaka, alisema timu yenye jumla ya watu 22 itaondoka alfajiri ya kesho kuelekea Mwanza kwa ajili ya mashindano hayo.

Katibu Tawala huyo wa Mkoa  amesema mkuu wa mkoa Queen Sendiga ameahidi kutoa zawadi ya shilingi milioni tano endapo timu hiyo itarejea na ushindi kutoka Mwanza.

Nahodha wa timu ya mpira wa miguu, Afisa Utumishi Faraji Hussein, ameahidi kuwa Manyara itarejea na ushindi mkubwa akisema wachezaji wamejiandaa vizuri na wanalenga kuhakikisha wanapata bonasi hiyo ya milioni tano kutoka kwa Mkuu wa Mkoa.


Picha mbalimbali

















Post a Comment

0 Comments