Kikundi cha KIKURDI chateka vituo vya polisi na kuuwa watu kadhaa nchini UTURUKI

Serikali ya UTURUKI imesema kuwa wapiganaji wa kikurdi wamekamata vituo vya polisi vya nchi hiyo pamoja na kuua watu WATANO.

Wapiganaji hao wa kikurdi pia wamelipu bomu  wafanyakazi wa reli katika vituo viwili tofauti nchini UTURUKI.

Gavana wa jimbo la ADANA MUSTAFA BUYUK amesema wapiganaji wa PKK  wamelipua kituo cha polisi cha mjini POZANTI, na kuua maofisa wa polisi.

Katika upande wa mashariki wa jimbo la KARS, wapiganaji wa PKK  wamelipua mabehewa na baadae  kuwaua wafanyakazi wa reli ambao waliokuwa wakifanyia marekebisho reli hiyo katika eneo la ADEM UNAL na kuua mfanyakazi mmoja wa reli.

Ghasia kadhaa zimetokea nchini UTURUKI katika siku za hivi karibu baada ya kikundi cha wapiganaji cha PKK kuhusishwa na vifo vya maafisa wa polisi wa nchi hiyo katika mji wa SANLIURFA karibu kabisa na mpaka wa SYRIA.

Ghasia hizo zimesababisha serikali ya UTURUKI kutangaza mapambano dhidi ya kikundi hicho cha PKK kaskazini mwa IRAQ.


Waziri mkuu wa UTURUKI AHMET DAVUTOGLU amesema mashambulizi dhidi ya kikundi cha wapiganaji hao wa PKK hayataisha hadi pale wapinagaji hao wa PKK watakaposhusha chini mikono yao.
Mpya zaidi Nzee zaidi

Popular Items

Kilimo cha Bamia