Watoto wa familia moja wateketea kwa moto Mbeya


  Mbeya. Watoto wawili wa familia moja wameteketea kwa moto huku mama yao akiungua sehemu kubwa ya mwili wake baada ya chumba walichokuwa wamelala kuungua kwa moto katika Mtaa wa Itiji jijini hapa usiku wa kuamkia leo.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya , Ahmed Msangi amewataja watoto waliofariki  kuwa ni Raymond Erasto na Nestory Erasto (6) na kwamba mama yao aliyejeruhiwa ni Happy Erasto (26).

“Tukio hilo limetokea usiku wa kuamkia leo baada ya kibatari cha moto kuangukia godoro wakati watu wakiwa kwenye uzisingizi,” amesema kamanda Msangi

Kamanda Msangi amesema mama wa watoto walioteketea kwa moto, alijeruhiwa baada ya kujitosa kwenye moto ili awaokoe watoto wake na kwamba kwa bahati mbaya hakufanikiwa.

Tukio la watu kuungua mkoani Mbeya ni la pili baada ya mwishoni mwa mwezi Septemba kutokea tukio lingine wilayani Chunya ambapo mtoto Elizabeth Mwalupembe aliteketea kwa moto baada ya nyumba alimolala kuungua.
Mpya zaidi Nzee zaidi