Dida.
Dida ambaye miezi kadhaa iliyopita alivishwa pete ya uchumba na Mwenyekiti wa Kijiji cha Ukuni, Bagamoyo, Issa Seleman aliliambia Ijumaa Wikienda kuwa, hawezi kukurupuka kuingia kwenye ndoa kama zile za mwanzo kwani ana nia njema na ni kitu cha neema hivyo haihitaji kuwa na haraka.
“Siwezi kukurupuka tena kama ndoa za mwanzo, sina haraka kwa sasa, kuna vitu vinakamilishwa kwanza ndiyo maana uchumba wa muda mrefu,” alisema Dida.
